Tigo Yaja na Chapa Mpya
Honora Tanzania Public Limited (“Tigo”) na
Honora
Tanzania
Mobile Solutions Limited (“Tigo Pesa”), ambazo ni sehemu ya kampuni ya AXIAN
Telecom
Group
zinatangaza mabadiliko makubwa ya chapa ambapo Tigo itajulikana rasmi kama Yas,
huku
huduma zake
za kifedha, Tigo Pesa, zikibadilishwa kuwa Mixx by Yas. Hatua hii muhimu katika
historia
ya kampuni,
na inaakisi azma yake ya kuendeleza ubunifu wa kidijitali na ujumuishaji wa
Watanzania
kwenye
huduma za kifedha.
Mabadiliko
haya ya chapa ni sehemu ya mpango mkakati wa AXIAN Telecom wa kuunganisha
makampuni
yake yote ya mawasiliano barani Afrika kuwa chini ya chapa moja, Yas na Mixx by
Yas kama
alama ya nguvu
ya Pamoja na mafanikio.
Yas na Mixx
by Yas, zinalenga kuakisi maono ya kampuni ya kuwa kiini cha mapinduzi ya
kidijitali barani
Afrika.
Kupitia suluhisho za kisasa za kidijitali na kifedha, chapa hizi mpya zinalenga
kuboresha maisha ya
mamilioni ya
Watanzania na kutoa fursa mpya zisizo na kikomo.
Rostam
Azizi, Mwenyekiti wa Bodi ya Yas Tanzania, alisema;
“Yas ni
ishara ya nguvu tuliyonayo Afrika. Mabadiliko haya yanaonesha dhamira yetu ya
kuendelea
kuwekeza na
kuleta mageuzi ya kidijitali nchini Tanzania, bara na Visiwani. Tukishirikiana
na Axian
Telecom
Group, tumejipanga kutengeneza fursa mpya, kuhamasisha ubunifu, na kujenga
mustakabali
bora ulio na
lengo la kuimarisha sekta ya mawasiliano.”
Hassanein
Hiridjee, Mwenyekiti wa Bodi ya Axian Telecom Group, alisema:
“Axian
Telecom imekuwa katika safari ya kipekee ya kuunganisha watu barani Afrika
kupitia chapa zetu.
Kadri
tunavyopanua wigo wa humuma zetu, tunaendelea kuyafikia maono yetu ya kuwa
kampuni ya
mawasiliano
inayotoa hukduma kwenye nchi nyingi zaidi barani Afrika. Tunapozindua chapa
mpya ya
Yas,
tunalenga kuunganisha bara hili kwenye fursa mbalimbali. Tunaamini Yas
itaendeleza mafanikio na
utamaduni
wetu huku ikitoa suluhisho jumuishi na endelevu za kiteknolojia.”
Jerome
Albou, Kaimu Afisa Mkuu wa Yas Tanzania, aliongeza:
“Leo ni siku
ya kihistoria kwa kampuni yetu. Kama Yas, tumejipanga kuwa mshirika wa
maendeleo,
tukiwapa
nguvu wateja wetu na kuwahakikishia kuwa biashara zitastawi katika mazingira
yenye
ushindani
mkubwa. Hivyo basi tutaendelea kuwekeza katika teknolojia za kisasa, huduma
bora kwa
wateja huku
tukiendelea kuwekeza kwa vijana ambao ni msingi wa maendeleo ya baadaye ya
Tanzania.”
Mbali na
kuunganisha chapa zake za makampuni ya mawasiliano , Axian Telecom pia
inaunganisha
huduma zake
za kifedha nchini Togo, Senegal, na Tanzania chini ya chapa ya Mixx by Yas .
Lengo ni
kuboresha
uzoefu wa wateja kwa kushirikiana zaidi kati ya nchi hizi. Huduma za kifedha
kwa njia ya simu
za mkononi
ni eneo muhimu la ukuaji kwa kampuni barani Afrika, ikibaki mstari wa mbele
katika
ujumuishaji
wa kifedha.
Mabadiliko
haya yanaonesha azma ya Axian Telecom Group ya kuendelea kuboresha huduma zake
kwa
kutumia
teknolojia, ili kuwahudumia wateja wake vyema zaidi na kufanikisha maendeleo
endelevu
barani
Afrika.
Yas Tanzania
(zamani Tigo Tanzania) ni kampuni ya mawasiliano na teknolojia ya kidijitali
anayeongoza
nchini
Tanzania. Kwa zaidi ya miongo mitatu, Yas imekuwa mstari wa mbele katika utoaji
wa huduma za
kifedha
kupitia simu za mkononi, ikihudumia wateja zaidi ya milioni 23 kote nchini.
Ikiwa sehemu ya
Axian
Group—kinara wa huduma za mawasiliano barani Afrika—Yas inaongoza kuwa na
mtandao mpana
wa 4G
unaounganisha Watanzania kila kona ya nchi Pamoja na 5G yenye kasi zaidi. Huduma
za kifedha
kupitia simu
za mkononi za Mixx by Yas zinaendelea kuwezesha ndoto za watanzania kwa kuwa ni
salama, na
zinazopatikana kwa urahisi kila kona ya nchi.
No comments