Breaking News

RAIS MWINYI , WAZIRI JAFO WAITEMBELEA KAMPUNI YA TIGO

 

UGENI MZITO : Katika kuhitimisha maonesho ya 48 ya kimataifa ya biashara Kampuni ya Mtandao wa simu ya Tigo Tanzania imepata ugeni wa heshima katika banda lao baada ya kutembelewa na Rais wa Zanzibar Mheshimiwa Dk. Hussein Ali Hassan Mwinyi ambapo amejionea huduma mbalimbali zitolewazo na kampuni hiyo, Rais Mwinyi ameipongeza Tigo kwa juhudi zake na kufikisha huduma kwa jamii hasa wenye kipato cha chini kwa kuwafungulia dunia kupitia mawasiliano ikiwemo ofa mbalimbali na huduma za Kidigitali zitolewazo , Ikumbukwe  hivi karibuni Tigo wametambulisha simujanja ya ZTE A34 yenye uwezo wa 4G na inapatikana kwa bei nafuu ya Tsh, 650 kwa siku kwa mkopo ambapo kianzio chake ni elfu 35 tu , ikiambatana na MB 100 BURE kila siku kutoka Tigoni imara , Kioo chake inchi 6.6 , Kamera 2 , 64 GB Storage , Betri imara chaji hadi siku 2 " .
Kwa taarifa zaidi kuhusu OFA hii tembelea maduka ya Tigo kote nchini au mitandao yao ya kijamii .

No comments