Breaking News

Tanzania Commercial Bank yaungana na Standard Chartered Bank katika utoaji wa huduma za kibenki





Benki ya Standard Chartered Tanzania iliandaa hafla ya kiamsha kinywa kwa wateja wake wa Biashara katika Hoteli ya Hyatt Regency ikiwa pamoja na Benki ya Biashara Tanzania lengo ikiwa ni kuhamasisha huduma inayowawezesha wateja wa SCB kutumia mtandao wa TCB kuweka na kutoa pesa kwenye Matawi yake 82 pamoja na Wakala 5,600 wa TCB kote nchini.

Ushirikiano huu unalenga kutoa urahisi, wakati halisi na mazingira salama kwa wateja wa Standared Chartered Bank kutekeleza huduma zao za benki.

Katika Hafla hiyo ilihudhuriwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TCB, Bw. Jema Msuya pamoja na wawakilishi waandamizi kutoka benki hiyo, Rayson Foya, pamoja na Kaimukurugenzi wa Standared Chartered ambae pia ni Mkuu wa Kitengo cha Miamala Efeh Amoah pamoja na maafisa wengine kutoka SCB.

No comments