BENKI YA ABSA TANZANIA YADUMISHA USHIRIKANO NA WATEJA WAKE

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kushoto), Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Walid Alhad Omar, pamoja na wageni wengine wakichukua chakula cha futari katika hafla iliyoandaliwa na benki kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Walid Alhad Omar (kulia), akipokelewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, wakati wa hafla ya futari, iliyoandaliwa na benki kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Katikati ni Mdhibiti wa Masuala ya Fedha wa benki hiyo, Bw. Muhsin Kaye.

Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Ndabu Swere (wa tatu kushoto), pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa benki na wageni wengine, wakichukua chakula cha futari, katika hafla iliyoandaliwa na benki kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benkiy a Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, akiwahutubia wateja na wageni waalikwa, katika hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa wateja wake, jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Walid Alhad Omar, akihutubia baadhi ya wateja na wafanyakazi wa Benkiy a Absa Tanzania, wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Walid Alhad Omar (katikati), Mkurugenzi Mtendaji wa Absa Bank Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa pili kushoto), pamoja na baadhi ya wakurugenzi wa benki hiyo wakipiga picha ya pamoja baada ya hafla ya futari, iliyoandaliwa na benki kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Mdhibiti wa Masuala ya Fedha wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Muhsin Kaye (kushoto), akimuaga Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Walid Alhad Omar, huku Mkurugenzi Mtendaji wa benki, Bw. Obedi Laiser, akiangalia, baada ya hafla ya futari iliyoandaliwa na benki kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.



No comments